Wednesday, October 24, 2012

Messi, Xavi and Iniesta, World Soccer award finalists

The three Blaugranas are among the finalists for the best player of the year award given out by World Soccer magazine

 Messi current holder of the World Soccer award. PHOTO FCB.

 Three FC Barcelona players are among the ten candidates for the best player of the year award given out by World Soccer. Leo Messi, Xavi Hernández and Anrdés Iniesta will compete for the prize with Touré Yaya (Manchester City), Didier Drogba (Shangai Shenhua), Eden Hazard (Chelsea), Neymar (Santos) y Andrea Pirlo (Juventus), Cristiano Ronaldo (R.Madrid) and Radamel Falcao (At. Madrid).

Messi is the current holder of the World Soccer award, which he also won in 2009. Only the Brazilian Ronaldo, with three, has more editions of the prize. Ronaldinho also won back-to-back World Soccer awards in 2004 and 2005. The winner will be selected by the readers of the British magazine.

Xavi, 150 international games with Barça

The Catalan midfielder is the first player in the Club’s history to play 150 international matches

Xavi has figured in 129 Champions League, 13 UEFA Cup, 5 World Club Cup and 3 European Super Cup games
 PHOTO: MIGUEL RUIZ-FCB

 Xavi Hernández continues breaking Club records and this Tuesday he became the first Barça player to play in 150 international games. He made his debut on the European stage on September 16th 1998 at Old Trafford and has now gone on to make 129 Champions League appearances, as well as 13 in the UEFA Cup, 3 in the European Super Cup and 5 in the World Club Cup. In those 150 games, he has scored 12 times – 10  in the Champions League and once in the UEFA and World Club Cups.

Xavi is followed by an illustrious list of Barça players, including Puyol, Víctor Valdés, Iniesta, Migueli, Messi, Guardiola, Sergi, Zubizarreta and Cocu and also figures in the top ten European players with most international appearances. Paolo Maldini leads that group with 181 games played, followed by Raúl González, Clarence Seedorf, Javier Zanetti and Ryan Giggs, legends of European football who Xavi is fast catching up on.

Seven titles

Those 150 games have seen Xavi win three Champions League titles (2005/2006, 2008/09 and 2010/11), two European Super Cups (2009/10 and 2011/12) and two World Club Cups (2009/10 and 2011/12). Seven international titles to add to the seven league titles, two Spanish Cups and five Spanish Super Cups which he possesses and which have made him an outstanding figure in the Club’s history, with 641 appearances in all competitions for the team he has dedicated his career to.

Champions League ranking 2012 - 2013 Round 1

Champions League ranking 2012 - 2013 Round 1

 TeamsTotalHomeAway
 Group APointsPWDLSGCG  PWDLSGCGPWDLSGCG
1Oporto6220030 110010110020
2PSG3210142 110041100101
3Dinamo de Kiev3210134 110020100114
4Dinamo de Zagreb0200204 100102100102
 Group BPointsPWDLSGCGPWDLSGCGPWDLSGCG
1Arsenal6220052110031110021
2Schalke 044211043101022110021
3Montpellier1201134100112101022
4Olympiakos0200225100112100113
 Group CPointsPWDLSGCGPWDLSGCGPWDLSGCG
1Málaga6220060110030110030
2Milan4211032101000110032
3Anderlecht1201103100103101000
4Zenit St. Petersburgo0200226100123100103
 Group DPointsPWDLSGCGPWDLSGCGPWDLSGCG
1Real Madrid6220073110032110041
2Borussia Dortmund4211021110010101011
3Manchester City1201134101011100123
4Ajax0200215100114100101
 Group EPointsPWDLSGCGPWDLSGCGPWDLSGCG
1Shakhtar Donetsk7321052220041101011
2Chelsea4311174101022210152
3Juventus3303044101011202033
4Nordsjælland1301217201115100102
 Group FPointsPWDLSGCGPWDLSGCGPWDLSGCG
1Valencia6320162110020210142
2Bate Borisov6320165210134110031
3Bayern Munich6320144110021210123
4Lille0300316200214100102
 Group GPointsPWDLSGCGPWDLSGCGPWDLSGCG
1FC Barcelona9330073220053110020
2Celtic4311144101000210144
3Spartak Moscou3310267210144100123
4Benfica1301214100102201112
 Group HPointsPWDLSGCGPWDLSGCGPWDLSGCG
1Manchester U.9330063220042110021
2CFR 1907 Cluj Napoca4311143100112211031
3Sporting Braga3310245100102210143
4Galatasaray1301214201113100101

Tuesday, October 23, 2012

Manchester, Chelsea bado wababe


IMG_0133

Liverpool yachipua, Arsenal waoga kichapo


Marejeo ya Ligi Kuu ya England (EPL) baada ya mapumziko yamekuja na wimbi la ushindi kwa baadhi ya vigogo wa ligi hiyo.
Licha ya kuanza kujifunga, Manchester United walifanikiwa kusawazisha makosa yao na kuwachapa Stoke City mabao 4-2.
Majirani zao wamwaga fedha, Manchester City, wakicheza watu 10 walifanikiwa kukwepa kipigo kwa West Bromwich Albion kwa kusawazisha na kushinda 2-1.
Vinara wa ligi hiyo, Chelsea waliendelea kutoa dozi, nao wakitoka kwenye mbinyo wa mabao 2-1 hadi kushinda kwa 4-2 nyumbani kwa Tottenham Hotspur na kujitanua kileleni mwa ligi.
Arsenal waliwashangaza wengi kwa kukubali kichapo cha bao 1-0 walipocheza nyumbani kwa Norwich City ambao tangu kuanza ligi hawajafanya vyema.
Lakini wana Anfield, Liverpool walikuwa na la kujivunia, baada ya kupata ushindi wa kwanza wa ligi nyumbani.
Lilikuwa bao la chipukizi Raheem Sterling anayeanza kujihakikishia namba katika kikosi cha kwanza, lililoondoa mkosi kwa Wekundu hao kwa kuwakandika Reading bao 1-0.
Wigan wameendelea na matatizo yao kwa kukandikwa mabao 2-1 na vijana wa Swansea waliokuwa wameanza kusinzia baada ya kuanza vyema msimu huu.
Ufufuko wa Southampton kwa upande mwingine, ulionekana kuwa geresha tu, pale walipokubali kisago cha mabao 4-1 kutoka kwa West Ham United ya Sam Allardyice.
Utata wa Aston Villa uliendelea, baada ya kuadhiriwa kwa kufungwa bao 1-0 na Fulham katika mzunguko huu wa nane wa EPL.
Edin Dzeko alikuwa shujaa wa mabingwa watetezi, Manchester City, kwani aliingia na kupachika mabao mawili katika dakika za mwisho mwisho na kuwanusuru City kupata kichapo cha kwanza cha ligi.
City walijikuta katika wakati mgumu baada ya James Milner kupata kadi nyekundu mapema, ikiwa ni ya kwanza tangu aanze kucheza soka, kutokana na rafu mbaya dhidi ya mshambuliaji wa West Brom,
Shane Long aliyekuwa anakwenda kufunga.
Wayne Rooney alijifunga mwenyewe kabla ya kuifungia Manchester United mabao mawili katika ushindi dhidi ya Stoke uwanjani Old Trafford.
Wengine waliofunga kwa United ni Robin Van Persie na Danny Welbeck.
Chelsea walibadili mchezo kwa mabao mawili ya haraka haraka ya Juan Mata yaliyofanya matokeo yasomeke 3-2 kabla ya Daniel Sturridge kuingia dakika za mwisho na kufunga bao la nne.
Andre Villas-Boas alitumia kila silaha aliyokuwa nayo kuwaadhibu mahasimu waliomfukuza kazi Machi mwaka jana.
Hata hivyo, alichopata ni mabao mawili tu kutoka kwa beki William Gallas na Jermain Defoe.
Kichapo cha Arsenal ni cha pili msimu huu, tena katika mechi tatu tu, safari hii ikiwa mikononi mwa Norwich ambao ni ushindi wa kwanza.
Ajabu ni kwamba Norwich walipachika bao dakika ya 19 tu ya mchezo kupitia kwa Grant Holt, na Gunners wakashindwa kulikomboa, licha ya kucheza kikosi kamili.
Kocha Brendan Rodgers wa Liverpool alikuwa katika bahari ya majaribu tena, kwani alikuwa akikabiliana na timu aliyoifundisha siku zilizopita.
Sterling anayechezea pia timu ya taifa alimng’arisha kwa kupachika bao kutokana na pasi nzuri ya mshambuliaji mwandamizi pekee aliyebaki kikosini, Luis Suarez.
Sterling anaweka historia ya kuwa mfungaji mwenye umri mdogo zaidi wa Liverpool baada ya Michael Owen. Sterling ana umri wa miaka 17 na ana asili ya Jamaica, japokuwa ameamua kuchezea timu ya taifa ya England.

Hakuna suluhu ubaguzi katika soka England..

IMG_0283



Wachezaji wamewatolea uvivu viongozi wao

Swansea, Wigan wagomea fulana za kampeni

Rio, Roberts, Pienaar, Cisse, Lescott vinara

Sakata la ubaguzi wa rangi kwenye soka limeingia hatua mpya, baada ya wachezaji kadhaa weusi kuwatolea uvivu wanafiki.
Mshambuliaji wa Reading, Jason Roberts, Mwingereza mwenye asili ya Grenada alivunja ukimya kwa kukataa kuvaa fulana inayoashiria upigaji vita ubaguzi huo.
Aliungwa mkono na wachezaji zaidi ya 30, akiwamo Rio Ferdinand wa Manchester United, wanaoamini kwamba taasisi ya Kick It Out haijachukua hatua stahili kuukabili ubaguzi. Imekuwa utamaduni kila Oktoba kuadhimishwa wiki ya kupinga ubaguzi, na wachezaji wote walitarajiwa kuvaa fulana hizo kwa wiki moja kuanzia Oktoba 18.
Matukio haya yamekuja baada ya John Terry wa Chelsea kumbagua Anton Ferdinand (mdogowe Rio anayechezea Queen Park Rangers – QPR) na Luis Suarez wa Liverpool kumtolea lugha ya aina hiyo Patrice Evra wa United, kisha kukataa kumpa mkono mara mbili.
wachezaji waliokataa kuvaa fulana hizo kabla ya mechi za mwisho wa wiki ni Victor Anichebe, Sylvain Distin na Steven Pienaar wa Everton waliokuwa wakipambana na QPR.
Wenyeji wao, yaani QPR waliokataa fulana hizo ni
Anton Ferdinand kama alivyotarajiwa, Djibril Cisse, Shaun Wright-Phillips, Nedum Onouha na Junior Hoilett.
Jumamosi wachezaji wengi zaidi waligombea fulana hizo, nao ni Micah Richards na Joleon Lescott wa Manchester City na Rio Ferdinand wa Manchester United.
Mwassi wa mgomo huo alitimiza azma yake katika uwanja wa Anfield, naye ni Jason Roberts wa Reading wakati Kenwyne Jones wa Stoke naye aliitupa mbali fulana hiyo.
Swansea na Wigan walionesha mshikamano wa ajabu kwani wachezaji wao wote hawakuvaa fulana hizo.
Hatua ya wachezaji hao kukacha fulana zenye nembo yenye maneno ya Kiingereza; ‘Mchezo Mmoja Jamii Moja’ imekuja baada ya Ashley Cole wa Chelsea pia kumtetea mshirika wake Terry kortini.
Cole ambaye ni mweusi aliku kubezwa na Chama cha Soka (FA) cha Uingereza kwa vile ushahidi wakeu ulikuwa wa uongo, naye akajibu kwa kuwatusi maofisa wa FA.
Matokeo ya hatua yake ya kiburi na majigambo imeishia kutozwa faini ya Pauni 90,000. Rio amemfananisha Cole na ‘choc ice’, yaani barafu ambayo nje huweza kuwa nyeupe na ndani nyeusi. Rio alipigwa faini ya Pauni 45,000.
Terry aliadhibiwa kulipa faini ya Pauni 220,000 na kukosa mechi nne za ligi, akadai angekata rufaa.
Hata hivyo, mwishoni mwa wiki iliyopita amesema hatakata rufaa, hatua inayoonesha ameridhia adhabu zote na anajua kwamba alifanya makosa ya ubaguzi wa rangi dhidi ya Anton.
FA ilimwadhibu Suarez kukosa mechi nane na kulipa faini ya Pauni 40,000 kwa makosa yake ya kujirudia rudia. Chelsea nao wamemwongezea Terry adhabu na walisema Cole naye angeadhibiwa, lakini Terry anabaki nahodha wa mabingwa hao wa Ulaya.
Wakati hatua hizo zikichukuliwa, taasisi ya Kick It Out inachukuliwa na wachezaji weusi kwamba imelemaa na haijakuwa makini kushughulikia tatizo hilo, hivyo wakaamua kuachana na fulana zao, ili walau kufikisha ujumbe.
Wakati makocha wa timu ambazo wachezaji wao waligomea fulana hizo wakionesha upole, Kocha wa Manchester United, Alex Ferguson aligeuka mbogo, akidai Rio angeshughulikiwa.
Lakini ni Rio huyo huyo anayetegemewa na klabu yake katika ulinzi Jumanne hii katika hatua za mtoano za Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Jumatatu asubuhi, Rio na Ferguson walionekana mazoezini, wote wakitabasamu na kujenga hisia kwamba hapangekuwa na adhabu yoyote.
Yalichapishwa madai mwishoni mwa wiki, kwamba huenda Rio angeadhibiwa kwa kukatwa mshahara wa wiki mbili, ambao ni Pauni 220,000, na hatima yake Man U kuwa shakani. Si rahis kwa kocha Ferguson kuchukua hatua kama hiyo.
Hata angeadhibiwa Rio ni mtu wa msimamo na katika masahibu ya mdogo wake na mengine ya wanaodhalilishwa, amekuwa nao siku zote, bila kuogopa kitakachompata.
Pengine ni kwa sababu hiyo, Ferguson amekengeuka na kusema kwamba hakuna tatizo kati yake na Rio na kwamba mambo yote yameshawekwa sawa.
Akizunguza na waandishi wa habari Jumatatu alasiri, Ferguson alisema kwamba kilichotokea ni ukosefu wa mawasiliano kutoka kwa Rio, aliyetarajiwa kutoa notisi ya kusudio la kutovaa fulana hiyo.
Ferguson alionekana kuudhika, hasa kwa sababu alikuwa amemshambulia Roberts wa Reading kwa kutangaza kugomea uvaaji fulana, akisema kwamba mshambuliaji huyo hakuwa na hoja.
‘Kick Racism out of Football’ ilianza mwaka 1993 kabla haijabadilika na kuwa ‘Kick It Out’ mwaka 1997.
Katika msimu wa mwaka 2010/11 taasisi hiyo ilikuwa na bajeti ya £453,913. Kati ya hizo, £330,000 zilitolewa na FA, taasisi inayoendesha Ligi Kuu na Chama cha Wanasoka wa Kulipwa (PFA).
Akizungumzia suala la ubaguzi kwenye soka, Mark Hughes – Kocha Mkuu wa QPR anayochezea Anton Ferdinand anasema itachukua muda mrefu kumaliza tatizo hilo.
Kocha wa Everton, David Moyes anawaunga mkono wachezaji wake watatu kwa walilofanya, japokuwa anasema kwamba hiyo haina maana anakubaliana na hoja yao.
Ni vigumu kwa kocha yeyote mweledi kuwaadhibu wachezaji weusi kwa sababu eti wamekataa kuvaa fulana hizo, kwa sababu wapo wanaowatukana mara nyingi wasioadhibiwa. Itachukua muda kupata suluhu katika hili.

Tuesday, October 16, 2012

Safari ya Cole inafika mwisho Chelsea?

IMG_0147

Vidic naye adaiwa kuaga Manchester United


Beki wa kushoto aliyepata kudaiwa kuwa bora zaidi duniani, Ashley Cole anakaribia kuondoka Chelsea.
Mchezaji huyo aliyeichezea England mechi 98 tayari anawindwa na klabu tatu kubwa.
Mkataba wa Cole unaisha mwisho wa msimu huu, ambapo inadaiwa kwamba amepewa ofa ya mkataba wa mwaka mmoja tu asioutaka, kama ilivyokuwa kwa Didier Drogba.
Sera ya Chelsea imekuwa kwamba hakuna kutoa mkataba wa zaidi ya mwaka kwa wachezaji wenye umri wa zaidi ya miaka 30, na Cole anayo 31.
Habari hizi zinakuja wakati beki huyo akiomba huruma ya Chama cha Soka (FA) England baada ya kuwatukana maofisa wake kwa kutumia mtandao jamii.
Cole alikasirishwa na jinsi FA kubeza utetezi wake kwa John Terry aliyemtusi kibaguzi Antony Ferdinand wa Queen Park Rangers (QPR). FA ilisema Cole ni mwongo na ushahidi wa Terry ulikuwa wa kutunga.
Wakati safari ya Cole ikikaribia ukingoni Stamford Bridge kama Drogba anayecheza China, makocha wake wa zamani, Jose Mournho wa Real Madrid na Carlo Ancelotti wa Paris Saint-Germain wanadaiwa kusubiri kumchukua.
Ni Ancelotti aliyetangaza hivi karibuni kwamba Cole ndiye beki bora zaidi wa kushoto, na kwamba klabu inayotaka uimara lazima imtafute.
Hata hivyo, si ajabu Cole asiondoke kwenye Ligi Kuu, kwani Kocha Mkuu wa Manchester United, Alex Ferguson anadaiwa kumtaka Cole siku nyingi.
Kama alivyomnyakua Robin Van Persie wa Arsenal mkataba wake ulipokaribia kumalizika Emirates, Ferguson anaelekea kunyatia mazingira ya Chelsea na Cole ili Januari aingie Old Trafford.
Lakini, kwa upande mwingine inadaiwa kwamba Cole anatikisa tu kiberiti wala hana mpango wa kuondoka, bali ni namna ya kupata mkataba mrefu au fedha nyingi zaidi Stamford Bridge.
Watu wa karibu naye wanasema kwamba Chelsea wanatakiwa kuonesha heshima kwa Cole kwa mchango aliotoa kwa timu hadi kutwaa kombe la Ulaya, kwani umri haujamzuia kucheza vyema.
Iwapo Cole ataamua kuondoka Chelsea kwa sababu zozote, kuna uwezekano wa nafasi yake kuchukuliwa na Benoît Assou-Ekotto wa Tottenham Hotspurs.
Taarifa zaidi kuhusu kuhama wachezaji zinamgusa nahodha wa Mashetani Wekundu, Nemnaja Vidic anayehusishwa na kuhamia klabu ya Kirusi inayomwaga noti, Anzhi Makhachkala, inayotaka kumpa mshahara wa Pauni milioni 12 kwa mwaka baada ya kodi.
Hata hivyo, si rahisi kwa Ferguson na United kwa ujumla kumwacha beki huyo wa Serbia aliyerejea uwanjani baada ya kuwa majeruhi kwa muda mrefu aondoke, kwani ni nguzo kubwa ya safu yao ya ulinzi.

Kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

13 WAPITISHWA KUGOMBEA UONGOZI TWFA

 normal_2Ofisi_Mpya_za_Shirikisho_La_Mpira_Wa_Miguu_Tanzania_TFF

Wagombea 13 kati ya 15 waliojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) wamepitishwa baada ya usaili uliofanyika juzi.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TWFA, Ombeni Zavala, waliopitishwa kwenye nafasi ya uenyekiti ni Isabellah Huseein Kapera, Joan Ndaambuyo Minja na Lina Paul Kessy.
Makamu Mwenyekiti ni Rose Kisiwa wakati wanaowania nafasi ya Katibu Mkuu ni Amina Ali Karuma na Cecilia Oreste Makafu. Mgombea pekee wa nafasi ya Katibu Msaidizi, Macky Righton Mhango naye amepita kwenye usaili huo. Aliyepitishwa kwenye nafasi ya Mhazini ni Rose Stewart Msamila.
Furaha Francis na Zena Chande wamepitishwa kuwania nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wakati waliopita kuwania ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya TWFA ni Triphonia Ludovick Temba, Rahim Salum Maguza na Sophia James Charles.
Hivi mchakato wa uchaguzi wa TWFA uko katika kipindi cha kukata rufani ambapo ni kuanzia Oktoba 15-17 mwaka huu. Rufani zinatakiwa zifike kwa Katibu Mkuu wa TFF kabla ya saa 10 kamili jioni ya Oktoba 17 mwaka huu.
Wagombea wawili ambao hawakupitishwa kwa ajili ya uchaguzi huo
unaotarajiwa kufanyika Novemba 4 mwaka huu ni Julliet Mndeme na Jasmin Soud walioomba ujumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF. Wagombea hao ambao pia walikuwa wamewekewa pingamizi hawakufika kwenye usaili.

PONGEZI KWA UONGOZI MPYA ARFA


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi kwa uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika jana (Oktoba 14 mwaka huu).
Ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa COREFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo mkoani Pwani.
TFF inaahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya COREFA chini ya uenyekiti wa Hassan Othman Hassan ambaye amechaguliwa tena kuongoza chama hicho.
Uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu mkoani Pwani kwa kuzingatia katiba ya COREFA pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yake.
Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya COREFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi za wanachama wa TFF.
Viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni Hassan Othman Hassan (Mwenyekiti), Riziki Majala (Katibu), Geofrey Irick Nyange (Mjumbe wa Mkutano Mkuu TFF), Juma Haruna Kisoma (Mwakilishi wa Klabu TFF) na Abubakar Allawi (Mhazini).
Waliochaguliwa kuwa Wajumbe wa Kamati ya Utendaji katika uchaguzi huo uliofanyika kisiwani Mafia ni  Musa Bakari Athumani, Godfrey Magnus Haule na Gwamaka Oden Mlagila. Mwakilishi wa Wanawake ni Florence Ambonisye.

Monday, October 15, 2012

NYERERE VOLLEYBALL MEMORIAL CUP- NOVEMBER 15 TO 18 MOSHI TANZANIA

Picha_mseto_no2_036

Tanzania Volleyball Association is currently in the preparations for this year’s Mwalimu Nyerere Memorial Volleyball Cup.

The championship scheduled from November 15 ,winds up on 18,2012 at Hindu Mandal Volleyball courts in Moshi is expected to draw teams from neighboring Kenya, Uganda, Rwanda and Burundi.
Currently the Cup holders Jacaranda Volleyball Club from Mombasa Kenya have confirmed participation on this prestigious event.
Other local teams who have confirmed participation include Tanzania Prisons who have recently clinched National Club title, Jeshi Stars men and women, Mzinga, Kili Stars Tanzania Prisons Women, Dodoma and Morogoro Stars.

Teams from Rwanda and Burundi have been invited for the first time just to make the tournament more East African affair.
Mwalimu Nyerere Volleyball Memorial Cup is an annual event   made in the memory of the founder and father of the nation Tanzania.
Mwalimu Nyerere vigorously struggled for the unity of Africa and the World at large before his death 13 years ago.
Mwalimu Nyerere was at one time ready to delay Tanganyika Independence until Kenya and Uganda gets their Independence first.
Mwalimu Nyerere also a founder of PAN AFRICANISM / PAFMECA was always in support of the poor citizens and totally against corruption which is currently being practiced by most of our leaders.
Tanzania Volleyball Association has in the past 12 years organizing an annual volleyball memorial Cup in his remembrance to advocate the good deeds he made for Tanzania, Africa and the World at large
Through sports we believe we can make his dreams come in reality and this is why we have invited Rwanda and Burundi teams to join with teams from Kenya, Uganda and hosts Tanzania in strethening East Africa, simply a milestone towards African unity.

Mabingwa Zambia wapita kwa mbinde *Uganda wawabana pumzi hadi penati 20


IMG_0223 


Mabingwa wa Afrika wamefuzu kushiriki Kombe la Mataifa ya Afrika kwa bahati, baada ya kuzidiwa nguvu katika dakika 90 za mchezo.
Uganda ndio waliowafanya Zambia wakeshe wakiomba, baada ya kuwatungua kwa bao moja jijini Kampala.
Hiyo ilikuwa kulipiza kisasi kwa Zambia waliowachapa bao hilo hilo mjini  Ndola, Zambia mwezi uliopita.
Timu ya kufuzu kushiriki mashindano hayo yatakayofanyika Afrika Kusini hakuweza kupatikana, hata baada ya Zambia na Uganda kupigiana penati tano tano, kwani walikuwa nguvu sawa.
ilibidi mikwaju zaidi ya penati iongezwe hadi mshindi apatikane, ndipo ikabidi mabingwa waende hadi penati ya 10 ili kupata ushindi, na sasa wana kazi kubwa ya kutetea kombe.
Wa Zambia ulikuwa ushindi wa penati 9-8, ambapo Patrick Ochan wa Uganda alikosa penati muhimu, katikati ya kelele za washabiki wa Uganda waliotaka kuona timu yao ikiingia kwenye fainali hizo.
Mechi hiyo ilijenga ushindani wa aina yake uliokaribia na uhasama, ambapo Uganda kwa mara nyingine wamekosa nafasi ya kufuzu kwa asilimia ndogo kabisa.
Kwa mpira ulivyoanza Jumamosi hii jijini Kampala, wakiwa na uungwaji mkono wa maelfu ya washabiki wao, Uganda walionekana kuwa na nafasi nzuri ya ushindi.
Na kweli, katika dakika ya 27 tu mambo yalijipa, kwani Geoffrey Massa aliandika bao la kuongoza, huku Uganda wakiwachezesha Zambia kwata na kuwafanya wahemee juu juu.
Uganda waliendelea kucheza kwa kujituma ili kutafuta bao la pili ambalo lingewahakikishia kufuzu moja kwa moja, lakini kikosi hicho kinachonolewa na Mskochi, Bobby Williamason kilishindwa kuwazidi nguvu mabingwa.
Golikipa wa Zambia, Kennedy Mweene atakumbukwa na Waganda, kwani alizuia nafasi zao za wazi za kuandika mabao, kushinda na kufuzu, kutokana na jinsi alivyocheza kwa ushujaa.
Nyota ilionekana kulalia kwa wenyeji bado, kwani wageni walipoanza kupiga penati, walikosa ya kwanza kupitia kwa nahodha wao, Chris Katongo.
itakumbukwa kwamba, Katongo ndiye alikuwa chachu ya ushindi uliowafanya Zambia kutawazwa mabingwa wa Afrika, hivyo alipewa nafasi ya kwanza akiaminika angefunga, ili awatie nguvu wenzake, lakini haikuwa hivyo.
Hata hivyo, Uganda walishindwa kutumia fursa hiyo kwa uendelevu, nao wakafikia mahali wakashindwa, hadi ilipofika fursa ya Ochan aliyeshindwa kufanya kweli.
Zambia walishinda mechi ya fainali ya kombe hilo mwaka huu kwa mikwaju ya penati dhidi ya Ivory Coast, katika fainali zilizofanyika Libreville, Gabon.
walihamasika kucheza vyema, maana fainali hizo zilifanyika karibu na ufukwe ambao wachezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Zambia walifia kwa ajali ya ndege mwaka 1993.
Uganda ilikosa ushiriki wa fainali zilizopita kwa ncha ya sindano, walipokwama kushinda mechi ya mwisho ya kufuzu iliyofanyika Kampala.
mara ya mwisho kushiriki fainali hizo ni 1978, ambapo walifika hadi fainali, wakaishia kuwa washindi wa pili.
Timu ya taifa ya Mali iliichapa Botswana mabao 4-1 na kujikatia tiketi ya kushiriki fainali hizo, katika mchezo uliofanyika kwenye uwanja uliokarabatiwa wa Lobatse.
 Magoli ya Mali yalifungwa na Cheikh Tidiane Diabate, Modibo Maiga, Mahamadou Samassa na Abdou Traore na kuwafanya Mali wawe na ushindi wa jumla wa mabao 7-1.
Mali walishika nafasi ya tatu kwenye fainali zilizopita.
Ghana walikuwa wa kwanza kufuzu kwa fainali hizo, baada ya mchezaji wao mahiri, Afriyie Acquah kufunga bao pekee kwenye mchezo wake dhidi ya Malawi uliofanyika mjini Lilongwe.
Acquah aliitwa kwenye kikosi hicho dakika za mwisho kuchukua nafasi ya majeruhi. Katika mchezo wa kwanza, Ghana walishinda mabao 2-0 nyumbani.
Timu hiyo ya Afrika Magharibi ilikuwa ikipewa nafasi kubwa kutwaa kombe mwaka huu, lakini waliishia nusu fainali, walipotolewa na Zambia.
Waliishia kushika nafasi ya nne, baada ya kupokea kichapo kutoka kwa Mali katika mechi ya kutafuta mshindi wa tatu.
fainali za Mataifa ya Afrika zinafanyika nchini Afrika Kusini kuanzia Januari 19 hadi Februari 10 mwakani, na ni moja ya michezo yenye mvuto barani Afrika na kwingineko.


Thursday, October 11, 2012

Uongozi wa mpira wa miguu unahitaji uamuzi mgumu-Tenga

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amezitaka Kamati za Uchaguzi kufanya kazi kwa kuzingatia Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF ili kuwa na uchaguzi huru na wa haki.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Dar es Salaam leo, Rais Tenga amesema uongozi wa mpira wa miguu unahitaji uamuzi mgumu, hivyo Kamati za Uchaguzi ambazo zimeundwa kwa mujibu wa Katiba zinatakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni na si kuangalia sura za watu.
Amepongeza kamati zilizosimamia uchaguzi kwa kufuata kanuni, na ingawa kila mtu ana haki ya kuongoza, jambo lolote lazima liwe na kanuni, kwani hata kwenye mikutano ya hadhara kuna kanuni.
“Huwezi kufika kwenye mkutano wa hadhara na wewe unaanzisha mkutano wako. Lazima kanuni ziheshimiwe ili kufanya uchaguzi uwe huru na wa haki. Nini kimetokea kwenye maeneo ambayo kuna matatizo? Kila mwanachama wetu (mkoa/chama shiriki) ana Kamati ya Uchaguzi ambayo imeundwa kwa mujibu wa kanuni.
“Zile kamati hazitekelezi majukumu yake, unampitisha mtu unajua hana sifa unasema acha akafie mbele (Kamati ya Uchaguzi ya TFF). Kanuni zinasema jaza fomu mwenyewe, weka nakala za vyeti na si kwamba huyu tunamjua. Kanuni zinatakiwa zifuatwe, ukienda kinyume unaondolewa,” amesema.
Amesisitiza kamati zifanye kazi kwa kufuata kanuni ili kusaidia mpira wa miguu kwani zimeundwa kihalali, kwa hiyo zisiogope kuengua hata walioziteua kama hawana sifa.
Pia Rais Tenga amezitaka Kamati za Utendaji na Sekretarieti kutoziingilia Kamati za Uchaguzi katika mchakato wa uchaguzi, badala yake zinatakiwa kuziwezesha tu (facilitation).
Amesema baadhi ya wagombea nao ni tatizo kwani wanaingia kwenye uchaguzi bila kuzielewa Katiba za vyama vyao na Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF, hivyo ni vizuri wakazielewa kwanza.
Rais Tenga amesema ni vizuri wanachama wote wakafanya uchaguzi kabla ya uchaguzi wa TFF utakaofanyika Desemba mwaka huu ili wapate fursa ya kupiga kura kwenye uchaguzi huo wa shirikisho.
Vilevile amewataka wadau kujitokeza kwa wingi kuwania uongozi kwenye chaguzi za vyama wanachama wa TFF, kwani mwitikio umeonekana kuwa mdogo kulinganisha na umaarufu wa mchezo wenyewe.
Amepongeza vyama vya mikoa ambavyo tayari vimefanya uchaguzi wao. Baadhi ya vyama hivyo ni Arusha, Dodoma, Iringa, Kagera, Kigoma, Kilimanjaro, Manyara, Mara, Morogoro, Mtwara na Singida.

Arsenal imefaidi kwa kumuuza RVP

DSC01788

*Wachezaji wana raha, wamejipanga upya

Robin Van Persie ameanza kusahaulika Arsenal, baada ya kuondoka majira ya kiangazi na kujiunga na Manchester United kwa dau la pauni milioni 24.
RVP aliondoka akiwa na hasira fulani na kukosa shukurani kwa waliomfikisha kileleni kisoka, akidai klabu imeshindwa kuweka sera madhubuti za kuleta vikombe Emirates.
RVP amefunga jumla ya magoli 96 katika mechi 200 za ligi, ambapo msimu uliopita ndio alikuwa bora zaidi, akifunga magoli 30.
Ameshaondoka na sasa anachezea Mashetani Wekundu, na wadau wa Arsenal hawakuchelewa kupiga hesabu za faida za muda mfupi na mrefu za kumuuza Mdachi huyo.

Klabu Imepata Fedha Nyingi

Kitita cha pauni milioni 24 ilikuwa fedha nzuri kwa mchezaji ambaye umri wake unakwenda, aliyekuwa amebakisha msimu mmoja tu kwenye mkataba na aliyekwishatamka hataki kubaki klabuni.
Arsenal wangeweza kumbakisha kwa nguvu hadi msimu uishe, lakini hangecheza kama alivyokuwa, na mbaya zaidi angeondoka bila klabu kupata senti tano muda wake ukaisha.

Amani Inajengeka na Kudumu Klabuni

Itakumbukwa kwamba, Robin hakuwa akipenda mchezaji mwingine mwenye uwezo kumshinda, na hata lawama zake kwamba klabu hainunui wachezaji hazikuwa za dhati.
Robin anajulikana wazi kwamba hakufurahia jinsi wachezaji wa aina ya Aaron Ramsey walivyokuwa wakipanda chati klabuni hapo, hadi Ramsey akaja kuvunjwa mguu na mlinzi wa Stoke City, Ryan Shawcross; sasa Ramsey amerejea na anachanua.
Baada ya Ramsey kuumia, Wenger hakusajili mchezaji kwenye namba hiyo, lakini Robin aliendelea kujiona kama mfalme na kutotaka yeyote amfikie.
Hata alipoanza ngebe za kuondoka, inasemwa hakufurahishwa na kusajiliwa kwa Podolski, mtu ambaye ni wazi ni msaada kwa klabu na timu.
RVP angebaki, wachezaji wenzake ambao walishajua tabia yake wangejihisi vibaya, kwamba yupo klabuni tu kwa sababu anatakiwa wala hachezi kwa kujituma.
Hali hiyo ingeweza kusababisha akabaki anasononeka muda wote, na timu ingepata hasara. Ni bahati mbaya amekwenda kwa mahasimu wa Arsenal kisoka, lakini pesa tamu.
Kuondoka kwa RVP kunafungua mwanya kwa kizazi kipya cha washinda mechi kujitokeza na kujipanga, maana watu wa nje walikuwa wakidai kila wanaposhinda kwamba Arsenal wanabebwa na RVP.
Kukosekana kwake kunawafanya wengine wajitokeze kuchangia mabao na ushindi kwa timu.
Wapo akina Theo Walcott, Alex Oxlade-Chamberlain, Lukas Podolski, Gervinho na Santi Cazorla.
Olivier Giroud ameanza mambo yake, lakini pia kuna kinda la miaka 17, Serge Gnabry aliyejumuishwa kwenye kikosi cha ligi ya mabingwa Ulaya.
Kuondoka kwake kumetupilia mbali mtanziko uliokuwapo kwa wengi juu ya hatima yake, au kwamba Arsenal haingeweza kusimama bila yeye, akifuata msururu wa nyota walioondoka kabla yake, japo wengine waliaga kwa heshima bila dharau.
Ukweli leo hii ni kwamba Arsenal wanajiona hawatetereki hata aondoke nani. Hakuna tena kigugumizi kama kilichotanda wakati RVP akitikisa kibiriti. Sasa timu inajisuka vyema, imeanza vizuri ligi japokuwa bado kuna maeneo ya kurekebisha.
Donge nono lililopatikana kwa kumuuza RVP linaweza kuwekezwa kwa kununua wachezaji wanaohitajika, maana Kocha Arsene Wengere amekuwa akishutumiwa wakati mwingine kwamba hatumii fedha.
Lakini usajili wa Cazorla anayesemwa kuziba kabisa pengo la Cesc Fabregas na pia kununuliwa kwa Lukas Podolski na Giroud kunaonesha Wenger yu tayari kutumia fedha akiona inafaa.
Uuzaji wa RVP ulitokea baada ya watatu hao kusajiliwa, kwa hiyo bosi wa Washika Bunduki wa London ana fedha kibindoni kwa ajili ya kuimarisha kikosi Januari au hata kiangazi kijacho.
Pauni milioni 20 zinaweza kununua chipukizi kadhaa au mchezaji mmoja sampuli ya Cazorla.

Nahodha Mpya Ataleta Mambo Mapya

Kuondoka kwa Robin kunafungua mwanya kwa nahodha mpya kuleta utambulisho tofauti klabuni, badala ya uhafidhina ule ule wa zamani.
Licha ya tabia yake ya kutotaka wengine kumfikia kisoka, japo wanampita, kama nahodha yalihitajika mabadiliko.
Leo yupo Thomas Vermaelen, na kawaida ni kwamba manahodha wote huongoza kwa mifano yao wenyewe. RVP alifanya hivyo kwa kufunga mabao, Vermaelen anakuja kivingine na kujenga timu bora zaidi ya ushindi.
Wakati kama huu mwaka jana, Arsenal walikuwa wameshachakazwa vibaya sana, kwa wingi wa magoli na mechi walizoshindwa kwenye ligi, tofauti na sasa ambapo wamepoteza kwa tabu mechi moja dhidi ya Chelsea.
Ndiyo maana inasemwa RVP alikuwa akidaiwa kuwabeba Arsenal – katika njia sahihi au potofu. Sasa yupo kepteni mpya, mwenye moyo, dhamira, ni msemaji na ana uzoefu, pasipo upungufu wa kiwango cha teknolojia, basi sura mpya ya Arsenal inachanua.
Ni kweli kwamba kunyanyua kombe kwa timu iliyotoka patupu kwa miaka minane kingekuwa kipindi kizuri mno cha mpito kwa Mbelgiji huyu.
Hata hivyo, inatosha tu kwa sasa kwamba timu inakwenda vizuri, na yeye anazo sifa za kuwa kwenye nafasi hiyo, wenzake wakimuunga mkono.